Habari

TUME YATAKIWA JENGA MFUMO WA KUSIMAMIA SKIMU ZA UMWAGILIAJI NCHINI.

TUME YATAKIWA JENGA MFUMO WA KUSIMAMIA SKIMU ZA UMWAGILIAJI NCHINI.
May, 10 2022

Waziri wa Kilimo Mheshimiwa Hussein Bashe ameitaka Menejimenti ya Tume ya Taifa ya Umwagiliaji kujenga mfumo imara wa kusimamia Skimu za Umwagiliaji nchini na kusisitiza kuwa kipaombele cha Wizara yake katika Mwaka wa fedha 2022- 2023 ni Umwagiliaji.

Akizungumza katika kikao kazi na Menejimenti hiyo jijini Dodoma,  Mheshimiwa Bashe ametaja vipaumbele vingine kuwa ni pamoja na kuandaa mfumo  wa kibiashara utakao weza kuzalisha faida inayotokana na  uwekezaji wa miradi mbalimbali inayowekezwa na Tume.

Mheshimiwa Bashe amesema Tume ihakikishe asilimia 50% ya bidhaa zitokanazo na mazao zinazalishwa nchini kupitia kilimo cha Umwagiliji ifikapo mwaka 2030 ambapo ameitaka Tume ya Taifa ya Umwagiliaji kujenga miradi mikubwa ya kimkakati ya Umwagiliaji.

 “Nataka Tume hii ifanye miradi ya Umwagiliaji kama tunavyo zindua miradi ya SGR, kama tunavyozindua miradi ya Stigler, tunahitaji miradi kama Stiglers kwenye Umwagiliaji”

 Mheshimiwa Bashe pia amesisitiza  Menejimenti pamoja na watumishi wa  Tume ya Taifa ya Umwagiliaji  kufanya kazi kwa bidii, weledi, ikiwemo  muda wa ziada ili kufanikisha malengo yaliyowekwa na Serikali kufikia Hekta Milioni Moja lakimbili (1,200,000) Mwaka 2025.

GCU