Historia
Tume ya Taifa ya Umwagiliaji imeanzishwa kwa Sheria Na.04 ya Taifa ya Umwagiliaji ya mwaka 2013 kama Taasisi ya Serikali inayojitegemea chini ya Wizara inayohusika na Umwagiliaji.Tume imepewa mamlaka ya kuratibu,kendeleza na kusimamia Maendeleo ya Sekta ya Umwagiliaji nchini. Shughuli za utendaji za kila siku husimamiwa na Mkurugenzi Mkuu chini ya usimamizi wa bodi yenye wajumbe 10.