Habari

UJENZI BWAWA LA MEMBE WAFIKIA 45.83%

UJENZI BWAWA LA MEMBE WAFIKIA  45.83%
Feb, 07 2023

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mheshimiwa Rosemary Senyamule ameitaka Tume ya Taifa ya Umwagiliaji kusimamia kwa makini ujenzi wa Bwawa la Membe linalojengwa Wilayani Chamwino na kuhakikisha kuwa bwawa hilo linakidhi vigezo vinavyotakiwa ili lidumu kwa muda mrefu.

Membe Dam


Akizungumza na baadhi ya wanavijiji watakao nufaika na Bwawa hilo wakati wa ziara ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa bwawa katika eneo la mradi, mkuu huyo wa Mkoa amewaeleza wananchi wa Membe hatua madhubuti zinazochukuliwa na serikali ya awamu ya sita katika  kuhakikisha Wilaya ya Chamwino na mkoa wa Dodoma kwa ujumla  unaondokana na tatizo la njaa kupitia kilimo cha umwagiliaji ambacho ni cha uhakika. 

Bwawa la Membe linatarajiwa kuwa na mita za ujazo wa Milioni 12, maji ya Bwawa hili yatatutumika kwa shughuli za umwagiliaji, mifugo na masuala mengine ya kijamii.

Usukaji nondo katika eneo linalojengwa tuta Bwawa la Membe.


Vijiji vitakavyonufaika na Bwawa hilo ni Membe, Chitabuli, Mlimwa, Dabalo pamoja na wakazi wa Tarafa ya Chilonwa.
Mradi wa Bwawa la Membe utaongeza ajira katika kilimo na kuinua uchumi kwa wakazi wa Mpwawa kupitia kilimo cha umwagiliaji ambapo wakulima watalima mara 2 au 3 kwa mwaka kutegemea na aina ya mazao.
Gharama za ujenzi ni Bilioni 12 na muda wa ujenzi ni miezi 12.

Kipande kilichomwagwa zege katika tuta Bwawa la Membe.

 

Eneo la tuta lililomwagwa zege iliyochomoza kutoka ardhini Bwawa la Membe.