Dira na Dhima

Dira

Kuwa Tume iliyo thabiti na endelevu yenye uwezo wa kuweka msukumo katika mageuzi ya sekta ya kilimo kuwa sekta imara na yenye kuhimili ushindani nchini.

Dhima

Kuendeleza miundombinu ya umwagiliaji kwa kuzingatia usimamizi wa pamoja wa rasilimali za maji ili kuleta ufanisi katika matumizi ya maji kwa lengo la kuwa na uzalishaji na tija endelevu, usalama wa chakula, kupunguza umaskini na kuleta maendeleo ya uchumi wa Taifa.