Fedha na Akaunti

Madhumuni

Kutoa huduma ya usimamizi wa masuala ya fedha na vitabu vya mahesabu ya fedha za Tume.

Kitengo hiki kitafanya kazi zifuatazo:-

Mishahara

(i) Kuandaa malipo ya Mishahara ikiwemo makato yakisheria;

(ii) Usimamizi wa malipo ya mishahara;

(iii) Kuandaa makisio ya masilahi ya watumishi;

(iv) Kuandaa Nyaraka za Pensheni; na

(v) Kutunza Kumbumbuku.

Ofisi ya malipo

(i) Kupeleka orodha ya nyaraka za malipoHazina;

(ii) Kuchukua hundi zote kutoka Hazina;

(iii) Kupeleka benki malipo ya fedha taslimu na hundi;

(iv) Kutayarisha taarifa ya fedha ya kila mwezi;

(v) Kuwalipa watumishi/wateja (watoa huduma) fedha taslimu au hundi;

(vi) Kutunza kwenye vitita vocha za malipo yaliyofanyika;

(vii) Kutunza vitabu vya malipo ya fedha taslimu;

(viii) Kutunza/kuwianisha malipo ya safari yaliyoidhinishwa; na

(ix) Kuandaa na kulipa malipo yote.

Mapato

(i) Kukusanya mapato yote;

(ii) Kusimamia mapato kulingana na kanuni na miongozo; na

(iii) Kufanya usiluhisho wa hesabu za Tume katika benki.

Penshseni

(i) Kuandaa Nyaraka za pensheni; na

(ii) Kutunza kumbukumbu za pensheni.

Bajeti

(i) Kuandaa bajeti;

(ii) Kufuatilia mgawanyo na matumizi;

(iii) Kuandaa hesabu za mwisho wa mwaka na taarifa nyinginezo zakifedha.

Ukaguzi waHesabu wa Awali

(i) Kukagua nyaraka za malipo ikiwa ni pamoja na idhini kulingana na taratibu;

(ii) Kukagua taratibu za kifedha na kuhakikisha zinaendana na sheria, kanuni, Nyaraka mbalimbali; na

(iii) Kujibu hoja zote za ukaguzi kwakipindi cha mwaka wa fedha uliopita.

Kitengo hiki kitaongozwa na Mhasibu Mkuu