Mawasiliano ya Serikali

Madhumuni

Kutoa utaalamu , huduma ya habari na mawasiliano kwa Tume; na kufanya majadiliano na umma na vyombo ya habari.

Kitengo hiki kitafanya kazi zifuatazo:-

(i) Kuandaa na kusambaza nyaraka kama vipeperushi, machapisho, makala za magazeti na kutaarifu umma juu ya sera, programu, majukumu na mageuzi yanayofanywa na Tume;

(ii) Kuratibu utoaji wa habari kwa ajili ya Tume;

(iii) Kushiriki katika mazungumzo na umma ikiwa ni pamoja na vyombo vya habari juu ya masuala yanayohusu Tume;

(iv) Kuendeleza programu za Ofisi;

(v) Kuratibu uandaaji wa machapisho ya Tume kwa ajili ya semina na mikutano;

(vi) Kuratibu uandaaji na uzalishaji wa machapisho na magazeti;

(vii) Kuboresha taarifa za ofisi kwenye tovuti ya Tume;

(viii) Kushauri juu ya uandaaji wa nyaraka mbalimbali; na

(ix) Kuandaa na kutekeleza mkakati wa mawasiliano wa Tume.

Kitengo hiki kitaongozwa na Afisa Habari Mkuu.