Teknolojia Habari na Mawasiliano

Madhumuni

Kutoa utaalamu na huduma juu ya matumizi ya TEHAMA kwa Tume.

Kitengo hiki kitafanya kazi zifuatazo:-

(i) Kutekeleza sera ya TEHAMA na Serikali-Mtandao;

(ii) Kuandaa na kuratibu mifumo ya usimamizi wa habari shirikishi katika Tume;

(iii) Kuhakikisha vifaa vya kompyuta na programu vinatunzwa vizuri;(iv) Kuratibu na kusaidia taratibu za manunuzi ya vifaa vya kompyuta na programukatika Tume;

(v) Kubuni, kuendeleza na kutekeleza udhibiti na kuhakikishausalama, uadilifu na upatikanaji wa habari;

(vi) Kuanzisha na kuratibu matumizi ya mawasiliano ya mtandao katika eneo husika (LAN and WAN); na

(vii) Kuandaa mafunzo na kupendekeza maeneo ya matumizi ya TEHAMA kama chombo cha kuboresha utoaji wa huduma katika ofisi yote.

Kitengo hikikitaongozwa na Mchambuzi wa Mifumo ya Compyuta Mkuu.