Usimamizi wa Manunuzi

Madhumuni

Kutoa utaalamu nahuduma juu ya manunuzi, utunzaji, ugavi wa bidhaa na huduma, na ufutaji wa mali chakavuza Tume.

Kitengohiki kitafanya kazi zifuatazo:-

(i) Kuishauri Menejemintijuu ya masuala yanayohusu manunuzi ya bidhaa na huduma, mbinu za usimamizi na ufutaji wa mali chakavu;

(ii) Kufuatilia uzingatiaji wa mchakato wa manunuzi na taratibu kwa mujibu wa sheria ya manunuzi na kanuni zake;

(iii) Kuandaampango wa manunuzi wa mwaka wa Tume;

(iv) Kufanya manunuzi na kufuta vifaa chakavu,kutunza na kusimamia ugavi, vifaa na huduma za kuendesha shughuli za Tume;

(v) Kutunza na kufuatilia mgawanyo wa mahitaji ya ofisi na vifaa;

(vi) Kutunza na kuboresha orodha ya bidhaa, mahitaji na vifaa;

(vii) Kutoa huduma za sekretarieti kwenye bodi ya manunuzi kwa mujibu wa sheria ya manunuzi na kanuni zake;

(viii) Kuainisha viwango/vipimo vya bidhaa na huduma zinazonunuliwa na kuhakikisha kuwa vinazingatiwa; na

(ix) Kuandaampango kazi, bajeti, nataarifa za utekelezaji wa kitengo.

Kitengo hiki itaongozwa na Afisa Ugavi Mkuu.