Mkuu wa Wilaya ya Tanganyika, Mhe. Onesmo Buswelu (katikati), akimwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Katavi, akikata utepe kuashiria uzinduzi rasmi na makabidhiano ya pampu za Umwagiliaji kwa wakulima wadogo mkoani Katavi. Pembeni yake ni Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Taifa ya Umwagiliaji (NIRC), Bw. Raymond Mndolwa (mwenye kofia na tisheti ya NIRC), pamoja na viongozi wengine wa Serikali na chama na baadhi ya wakulima.