

Nukuu ya Mhe. Rais Dkt, Samia Suluhu Hassan katika maadhimisho ya nanenane, viwanja vya John Mwakangale jijini Mbeya 2023

Nukuu ya Mhe. Rais Dkt, Samia Suluhu Hassan katika maadhimisho ya nanenane, viwanja vya John Mwakangale jijini Mbeya 2023

Picha ya Pamoja: Wataalamu wa Tume ya Taifa ya Umwagiliaji na Mkuu wa wilaya ya Tanganyika Mhe. Jamila Kimaro(wa tatu kutoka kushoto) wakati wa ziara ya timu hiyo ofisini kwake yenye lengo la kujenga uelewa wa pamoja kuhusu sheria ya Taifa ya Umwagiliaji na elimu ya ukusanyaji ada ya huduma za umwagiliaji.

Picha ya pamoja: Wataalamu wa Tume ya Taifa ya Umwagiliaji na mkuu wa wilaya ya Tanganyika Mhe. Onesmo Buswelu(wa katikati mstari wa mbele) wakati wa ziara ya timu hiyo ofisni kwake yenye lengo la kujenga uelewa wa pamoja kuhusu sheria namba 4 ya Umwagiliaji na elimu ya ukusanyaji ada ya huduma za umwagiliaji.

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Nsimbo Bw,Mohammedi Ntandu (aliyevaa miwani) akishauri jambo wakati wa mazungumzo baina yake na wataalamu wa Tume ya Umwagiliaji kujenga uelewa wa sheria namba 4 ya huduma za umwagiliaji na namna inavyotekelezwa katika skimu za umwagiliaji.

Picha ya pamoja: Timu ya wataalamu Tume ya Taifa ya Umwagiliaji na Mkuu wa mkoa wa Katavi Mhe. Mwamvua Mrindoko (wa pili kutoka kushoto) baada ya kujenga uelewa wa pamoja juu ya sheria ya taifa ya umwagiliaji na elimu ya ada ya huduma za umwagiliaji (wa pili kutoka kulia ni Mkuu wa kitengo cha sheria (Nirc) Bw, Andrew Rugarabamu.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akikata utepe kuashiria uzinduzi wa program mbalimbali za Taasisi mbalimbali zilizochini ya Wizara ya Kilimo ikiwemo zoezi la kuchimba visima vitakavyo Huduma wakulima 150 Kwa Kila Halmashauri nchini.

Mkurugenzi Mkuu Tume ya Taifa ya Umwagiliaji Bw. Raymond Mndolwa akimuonyesha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan utekelezaji wa programu ya kuchimba visima 1,840 kwaajili ya kuwahudumia wakulima wadogo.

Katibu mkuu kiongozi Balozi Dkt. Mosses Kusiluka akitazama miradi mbalimbali inayotekelezwa na Tume ya Taifa ya Umwagiliaji kwenye runinga.

Mkurugenzi Mkuu Tume ya Taifa ya Umwagiliaji Bw Raymond akimuonyesha katibu mkuu kiongozi Balozi Dkt Mosses Kusiluka mfano sa Miundombinu ya Bwawa (haupo pichani) wakati wa ziara ya kiongozi huyo katika banda la Tume ya Taifa ya Umwagiliaji maonesho ya 88 viwanja vya John Mwakangale jijini Mbeya.