

Wajumbe wa Menejimenti Tume ya Taifa ya Umwagiliaji na Wataalam wa Shirika la Maendeleo la Kimataifa la Japan (JICA) wakifuatilia taarifa ya Mpango kabambe wa Umwagiliaji (NIMP) katika ukumbi wa (Nirc) jijini Dodoma.

Mkurugenzi Mkuu (NIRC) Bw, Raymond Mndolwa akielezea hatua mbalimbali za utekelezaji wa miradi ya umwagiliaji kwa kipindi cha mwaka (2022 - 2023) na (2023 - 2024), mbele ya mgeni rasmi Waziri Mkuu Mhe, Kassim Majaliwa Majaliwa (Wa nne kutoka kushoto waliokaa)

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa, akizungumza katika hafla ya utiaji saini mikataba 20 ya ujenzi, ukarabati, upembuzi yakinifu na usanifu wa kina kati ya Tume ya Taifa ya Umwagiliaji na Wakandarasi 11 walioshinda Zabuni, ambapo amewaagiza watendaji wa (NIRC) kusimamia utekelezaji wa miradi hiyo kwa weledi na uaminifu mkubwa ili miradi hiyo idumu na kuwanufaisha wakulima.

Msimamizi wa mradi wa Regrow Skimu ya Madibira iliyopo Wilayani Mbarali Mkoa wa Mbeya, Mhandisi Njanji Mlwale(NIRC) akitoa tathmini ya maendeleo ya mradi huo kwa timu ya Ufuatiliaji na Tathimini kutoka Nirc Makao Makuu( kushoto kwa Mhandisi Mlwale ni Bw, Fredrick Mushi wa kitengo cha Manunuzi.(Kulia kwa Mhandisi Mlwale ni Mhasibu Jane Nyarusi na (aliyevaa Tshirt nyeupe ni Mhandisi Rebecca Momba) wakisikiliza kwa makini.

Kaimu Mkurugenzi wa uendelezaji miundombinu (NIRC) Mhandisi Mwinchuma Tengeneza (wa pili kutoka kulia) akitoa ufafanuzi wa jambo kwa Mwenyekiti wa Bodi ya (NIRC) Prof, Henry Mahoo (aliyevaa kofia ngumu rangi ya manjano wa kwanza kushoto). Wa kwanza kulia ni msimamizi wa mradi Bwawa la Membe Mhandisi Salehe Ahamadi. Kulia kwa Prof. Mahoo ni Mhandisi Machage Mwema (NIRC)

Mkurugenzi Mkuu (NIRC) Bw, Raymond Mndolwa (aliyevaa kofia rangi ya kaki) na Mkurugenzi wa uendelezaji miundombo (NIRC) Mhandisi Mshauri Fuko Koyoya (aliyevaa miwani ) wakikagua ujenzi wa daraja dogo barabara iendayo Shamba la (BBT) Ndogowe

Mkurugenzi Mkuu (Nirc) Bw, Raymond Mndolwa (aliyesimama) akiwakumbusha wahandisi wa umwagiliaji mkoa na wasimamizi wa miradi kuzingatia uandishi sahihi wa taarifa,uhifadhi wa kumbukumbu na nyaraka za kila siku katika utekelezaji wa miradi pamoja na kusimamia masharti ya mkataba, katika mafunzo ya kuwajengea uwezo yanayofanyika jijini Mwanza.

Mkurugenzi Idara ya Uendelezaji Miundombinu (Nirc) Mhandisi mshauri. Fuko Kuyoya (aliyesimama) akitoa mada katika mafunzo yakuwawezesha wahandisi wa umwagiliaji kupima kazi zao, kudhibiti ongezeko la kazi pamoja na kujua sheria na kanuni katika kufunga miradi mbalimbali ya umwagiliaji.

“Tunaendelea na uchimbaji wa visima na mabwawa katika maeneo mbalimbali nchini ili kufikia lengo kama tulivyoelekezwa na ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) ya kufikia ekari 1,200,000 za kilimo cha umwagiliaji ifikapo mwaka 2025,” Kauli ya Mkurugenzi Mkuu - Nirc - Bw,Raymond Mndolwa wakati wa kikao cha baraza la wafanyakazi mjini Dodoma.

Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu Wizara ya Kilimo, Hilder Kinanga awataka watumishi - NIRC -(Hawapo pichani) kufanya kazi kwa kuzingatia maadili na uadilifu ili kufanikisha azma ya Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, ya kuwezesha sekta ya kilimo c kuchangia asilimia 10 ya Pato la Taifa ifikapo mwaka 2030.