

Wajumbe wa kamati ya kudumu ya bunge ya kilimo, mifugo, biashara na viwanda wakikagua maendeleo ya ujenzi wa tuta la bwawa la Membe linalojengwa wilaya ya Chamwino Mkoani Dodoma.

Baadhi ya wajumbe wa kamati ya bunge ya kilimo, mifugo, biashara na viwanda wakikagua maendeleo ya ujenzi wa nyumba za mradi wa jenga kesho iliyobora (BBT) katika shamba kubwa (Block farm) lililopo Chinangali wilaya ya Chamwino mkoani Dodoma.

Wajumbe wa kamati ya kudumu ya Bunge ya kilimo,mifugo, viwanda na biashara wakikagua maendeleo ya ujenzi wa bwawa la Msagali linalojengwa wilayani Mpwawa. Gharama za ujenzi ni Tsh, bilioni 27, ujazo wa maji ni lita bilioni 92 na litamwagiliaji eneo lenye ukubwa wa hekta 4,500 sawa na hekari 11,250.

Mkurugenzi Mkuu Tume ya Taifa ya Umwagiliaji Bw, Raymond Mndolwa akiwaonyesha wajumbe wa Bodi ya Tume na Menejimenti hatua za ujenzi wa mfereji Skimu ya Mkombozi katika ziara ya wajumbe hao kukagua maendeleo ya ujenzi katika skimu hiyo. Skimu ya Mkombozi ina jumla ya Hekta 6000 na ujenzi wake unatarajiwa kukamilika mwaka 2024.

Mhandisi wa umwagiliaji mkoa wa Iringa Peter Akonaay akiwaeleza wajumbe wa Bodi ya Tume ya Taifa ya Umwagiliaji maendeleo ya utekelezaji ujenzi wa mradi Skimu ya Mkombozi kupitia michoro iliyowekwa kwenye bango.Wa pili kutoka kushoto ni Mwenyekiti wa Bodi Tume ya Taifa ya Umwagiliaji Prof. Henry Mahoo. Wa tatu kutoka kushoto ni Mkurugenzi Mkuu Tume ya Taifa ya Umwagiliaji Bw, Raymond Mndolwa. Wa nne kutoka kushoto ni Mkurugenzi wa uendelezaji miundombinu Mhandisi Mshauri, Koyoya Fuko.

Mwenyekiti wa Bodi Tume ya Taifa ya Umwagiliaji Prof. Henry Mahoo akifuatilia kwa makini mchoro wa Banio katika Skimu ya Mkombozi katika ziara ya Bodi na Menejimenti ya Tume katika Skimu ya Mkombozi mara baada ya kuhitimisha kikao cha Bodi.

Nukuu ya Mhe. Rais Dkt, Samia Suluhu Hassan katika maadhimisho ya nanenane, viwanja vya John Mwakangale jijini Mbeya 2023

Nukuu ya Mhe. Rais Dkt, Samia Suluhu Hassan katika maadhimisho ya nanenane, viwanja vya John Mwakangale jijini Mbeya 2023

Picha ya Pamoja: Wataalamu wa Tume ya Taifa ya Umwagiliaji na Mkuu wa wilaya ya Tanganyika Mhe. Jamila Kimaro(wa tatu kutoka kushoto) wakati wa ziara ya timu hiyo ofisini kwake yenye lengo la kujenga uelewa wa pamoja kuhusu sheria ya Taifa ya Umwagiliaji na elimu ya ukusanyaji ada ya huduma za umwagiliaji.

Picha ya pamoja: Wataalamu wa Tume ya Taifa ya Umwagiliaji na mkuu wa wilaya ya Tanganyika Mhe. Onesmo Buswelu(wa katikati mstari wa mbele) wakati wa ziara ya timu hiyo ofisni kwake yenye lengo la kujenga uelewa wa pamoja kuhusu sheria namba 4 ya Umwagiliaji na elimu ya ukusanyaji ada ya huduma za umwagiliaji.