Tanzania emblem
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Tume ya Taifa ya Umwagiliaji

Fedha na Akaunti

Madhumuni

Kutoa huduma ya usimamizi wa masuala ya fedha na vitabu vya mahesabu ya fedha za Tume.

Kitengo hiki kitafanya kazi zifuatazo:-

Mishahara

(i) Kuandaa malipo ya Mishahara ikiwemo makato yakisheria;

(ii) Usimamizi wa malipo ya mishahara;

(iii) Kuandaa makisio ya masilahi ya watumishi;

(iv) Kuandaa Nyaraka za Pensheni; na

(v) Kutunza Kumbumbuku.

Ofisi ya malipo

(i) Kupeleka orodha ya nyaraka za malipoHazina;

(ii) Kuchukua hundi zote kutoka Hazina;

(iii) Kupeleka benki malipo ya fedha taslimu na hundi;

(iv) Kutayarisha taarifa ya fedha ya kila mwezi;

(v) Kuwalipa watumishi/wateja (watoa huduma) fedha taslimu au hundi;

(vi) Kutunza kwenye vitita vocha za malipo yaliyofanyika;

(vii) Kutunza vitabu vya malipo ya fedha taslimu;

(viii) Kutunza/kuwianisha malipo ya safari yaliyoidhinishwa; na

(ix) Kuandaa na kulipa malipo yote.

Mapato

(i) Kukusanya mapato yote;

(ii) Kusimamia mapato kulingana na kanuni na miongozo; na

(iii) Kufanya usiluhisho wa hesabu za Tume katika benki.

Penshseni

(i) Kuandaa Nyaraka za pensheni; na

(ii) Kutunza kumbukumbu za pensheni.

Bajeti

(i) Kuandaa bajeti;

(ii) Kufuatilia mgawanyo na matumizi;

(iii) Kuandaa hesabu za mwisho wa mwaka na taarifa nyinginezo zakifedha.

Ukaguzi wa Hesabu wa Awali

(i) Kukagua nyaraka za malipo ikiwa ni pamoja na idhini kulingana na taratibu;

(ii) Kukagua taratibu za kifedha na kuhakikisha zinaendana na sheria, kanuni, Nyaraka mbalimbali; na

(iii) Kujibu hoja zote za ukaguzi kwakipindi cha mwaka wa fedha uliopita.

Kitengo hiki kitaongozwa na Mhasibu Mkuu