Tanzania emblem
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Tume ya Taifa ya Umwagiliaji

Idara ya Mipango, Ufuatiliaji na Tathmini

Madhumuni

Kutoa utaalamu na huduma katika mipango, bajeti, ufuatiliaji na tathmini.

Idara hii itafanya kazi zifuatazo:-

  1.  Kuratibu utayarishaji na utekelezaji wa mipango na bajeti ya Tume;
  2.  Kuhamasisha na kuwezesha utoaji huduma kwa sekta binafsi;
  3. Kutayarisha mchango wa ofisi katika taarifa ya bajeti na taarifa ya kiuchumi ya mwaka;
  4.  Kuweka mfumo wa utayarishaji wa mpango mkakati na kwa kuzingatia ujuzi wa kuandaa bajeti ya Tume;
  5. Kuratibu na kusimamia utekelezaji wa sera za Serikali;
  6. Kufanya uchambuzi wa sera za sekta mbalimbali na kutoa ushauri stahiki;
  7. Kufanya ufuatiliaji na tathmini katika mipango na bajeti ya Tume na kutayarisha taarifa za utekelezaji;
  8. Kutafiti, kuchambua na kufanya tathmini ya mipango kwa ajili ya kutoa maamuzi ya mwelekeo wa baadae wa Tume;
  9. Kuhakikisha kwamba mipango na bajeti ya Tume inajumuishwa katika taratibu za bajeti ya Serikali; na
  10. Kuratibu maandalizi na utekelezaji wa miradi / mipango ya maendeleo na upatikanaji wa rasilimali.
  11. Idara hii itaongozwa na Mkurugenzi na itakuwa na vitengoviwili kama ifuatavyo:

 

 Kitengo cha mipango; na Kitengo cha Ufuatiliaji naTathmini.

    1. Kitengo chaMipango

 

Kitengo hiki kitafanya kazi zifuatazo:-

  1. Kuratibu uandaaji na utayarishaji wa mpango wa mwaka na mpango mkakati wa muda wa kati;
  2. Kuweka pamoja miradi, mipango, mipango kazi na kuweka mikakati ya upatikanaji wa rasilimali;
  3. Kuwasiliana na Wizara ya Fedha na Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma juu ya michakato ya mipango mkakati na bajeti;
  4. Kutoa miongozo ya kitaalamu na kusaidia uwepo wa mpango mkakati na bajeti;
  5. Kushiriki katika uchambuzi wa kazi zisizo za msingi zinazoweza kufanywa na sekta binafsi; na
  6. Kutayarisha mkataba wa makubaliano kwa miradi na program yenye ufadhili wa kimataifa;

Kitengo hiki kitaongozwa na Mchumi Mkuu

1.2 Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini

Kitengo hiki kitafanya kazi zifuatazo:-

  1. Kufuatilia utekelezaji wa mpango wa mwaka wa Tume pamoja na mpango mkakati wa muda wa kati;
  2. Kutayarisha taarifa za utekelezaji wa mpango kwa vipindi maalumu (juma, mwezi, robo mwaka, nusu mwaka na mwaka);
  3. Kukusanya na kuchambua takwimu zinazohitajika katika utayarishaji na utekelezaji wa sera, mipango na mapendekezo ya bajeti;
  4. Kutoa mchango katika utayarishaji na uaandaji wa mipango na bajeti za Tume ikiwa ni pamoja na kuweka malengo muhimu na viashiria;
  5. Kutoa usaidizi wa kitaalamu ikiwa ni pamoja na kuweka mfumo wa ufuatiliaji na tathmini;
  6. Kufanya utafiti wa matokeo ya mipango, miradi na programu mbalimbali;
  7. Kufanya tathmini ya hali ya utoaji huduma kwa kukusanya maoni ya wadau juu ya huduma zinazotolewa; na
  8. Kuratibu mapitio ya utekelezaji wa mipango ya nusu mwaka na ya mwaka.

Kitengo hikikitaongozwa na Mchumi Mkuu