Tanzania emblem
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Tume ya Taifa ya Umwagiliaji

Ukaguzi wa Ndani

Madhumuni

Kutoa huduma zenyeuhakikana ushauri kwa Mkurugenzi Mkuu katika usimamizi bora wa Rasilimali fedha.
Kitengo hiki kitafanya kazi zifuatazo:-
(i) Kufanya mapitio na kutoa taarifa juu ya udhibiti sahihi wa mapokezi, uhifadhi na matumizi ya rasilimali fedha za Tume;
(ii) Kufanya mapitio na kutoa taarifa juu ya uzingatiaji wa taratibu za fedha zilizowekwa kwenye sheria ama kanuni au maagizo ya udhibiti wa matumizi ya fedha za Tume;
(iii) Kufanya mapitio na kutoa taarifa juu ya uainishaji na mgawanyo sahihi wa mapato na matumizi ya kihasibu; na
(iv) Kuandaa taratibu za kiukaguzi kulingana na Viwango vya Kimataifa;
(v) Kufanya mapitio na kutoa taarifa juu ya usahihi na ukweli wa kifedha na matumizi ya takwimu na kuandaa taarifa za kifedha na nyinginezo;
(vi) Kufanya mapitio na kutoa taarifa juu ya mfumo unaotumika kutunza rasilimali na kuhakiki uwepo wa rasilimali hizo;
(vii) Kufanya mapitio na kutoa taarifa juu ya utendaji au mipango ya kuhakiki ikiwa matokeo yanaendana na malengo na madhumuni yaliyokusudiwa;
(viii) Kufanya mapitio na kutoa taarifa juu ya maelezo ya Menejementiya Tume kwa ukaguzi wa ndani, nje, na taarifa ya tathmini ya nje na kuisaidia Menejeminti katika kutekeleza mapendekezo;
(ix) Kufanya mapitio na kutoa taarifa juu ya utoshelevu wa udhibiti wa mfumo wa kompyuta uliojengwa ndani ya Tume;
(x) Kutoa uhakika na huduma za ushauri wa namna ya kusimamia athari na michakatoya utawala bora;
(xi) Kuandaa mikataba ya huduma kwawateja juu ya shughuli za ukaguzi wa ndani na kamati ya ukaguzi.
(xii) Kuandaa mpango-mkakati wa kiukaguzi
Kitengo hiki kitaongozwa na Mkaguzi Mkuu wa ndani